JKCI Cycling Club yachangia damu kwaajili ya watoto wenye magonjwa ya moyo

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwa na wanachama wa klabu ya kuendesha baiskeli (JKCI cycling club) pamoja na kikundi cha waendesha baiskeli cha Twende Butiama jana kabla ya klabu ya JKCI cycling kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwaajili ya watoto wenye magonjwa ya moyo pamoja na kuchangia damu.


Wanachama wa klabu ya kuendesha baiskeli (JKCI cycling club) pamoja na wenzao wa kikundi cha Twende Butiama wakifanya maandamano ya baiskeli ya umbali wa kilometa 10 kabla ya kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwaajili ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa JKCI pamoja na kuchangia damu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na wanachama wa klabu ya kuendesha baiskeli (JKCI cycling club) pamoja na kikundi cha waendesha baiskeli cha Twende Butiama jana wakati klabu ya JKCI cycling ilipokuwa ikitoa msaada wa vitu mbalimbali kwaajili ya watoto wenye magonjwa ya moyo pamoja na kuchangia damu.



Wanachama wa klabu ya kuendesha baiskeli (JKCI cycling club) wakitoa msaada wa vitu mbalimbali kwaajili ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) jana jijini Dar es Salaam.

Wananchama wa klabu ya kuendesha baiskeli (JKCI cycling club) wakichangia damu kwaajili ya watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) jana baada ya kutoa msaada wa mahitaji mbalimbali kwa watoto hao.

Picha na: Hamis Mussa

***************************************************************************************************

Na Hamisi Mussa- Dar es Salaam

Klabu ya kuendesha baiskeli ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI Cycling club) imepongezwa kwa kuwakumbuka watoto wenye magonjwa ya moyo kwa kuwachangia damu pamoja na kuwapa zawadi za mahitaji mbalimbali.

Pongezi hizo zimetolewa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge alipokutana na kikundi hicho kabla ya kutoa zawadi na kuwataka kuendelea kuhamasisha michezo katika jamii ili waweze kijikinga na magonjwa ya moyo.

“Mmefanya ubunifu mkubwa kuanzisha klabu hii ya kuendesha baiskeli hapa JKCI, uongozi wa Taasisi unaungana nanyi kuhakikisha hiki mlichokianzisha kinakuwa kikubwa na kuhusisha wadau mbalimbali”, alisema Dkt. Kisenge

Dkt. Kisenge alisema kuendesha baiskeli ni sehemu ya michezo na michezo huchangia kuimarisha afya, jamii ikibuni vikundi mbalimbali vya michezo kama ambavyo JKCI inafanya itasaidia kupunguza magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo magonjwa ya moyo

“Nawashukuru sana kwakuweza kuwakumbuka watoto wetu wanaotibiwa JKCI kwa kujitoa kuchangia damu pamoja na kuwapa mahitaji mbalimbali ambayo ni ya muhimu kwao”, alisema Dkt. Kisenge

Kwa upande wake mwanachama wa klabu ya kuendesha baiskeli (JKCI Cycling Club) Henry Magwaza alisema klabu hiyo imeungana na klabu mbalimbali kuendesha baiskeli kwa pamoja na kushiriki kuchangia damu kwaajili ya watoto wanaotibiwa JKCI.

“Klabu ya kuendesha baiskeli ya JKCI (JKCI Cycling Club) tumeweza kutoa msaada wa mahitaji mbalimbali ya watoto wenye magonjwa ya moyo waliolazwa katika Taasisi hii tukiwa na lengo la kuonyesha upendo kwao”, alisema Henry

Henry alisema klabu hiyo imeamua kufanya matendo ya huruma kwa watoto hao kwani wamekuwa wakikaa wodini kwa muda mrefu na hivyo kuwa wapweke kutokana na maisha wanayopitia. 

 

 

  

Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Maabara ya JKCI yapata ithibati ya kimataifa (ISO 15189:2012)