JKCI yatoa mafunzo uchunguzi moyo wa watoto

 Madaktari bingwa wa magonjwa ya watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  Dkt. Stella Mongella  na John King’ori kutoka Hospitali ya Dian Beach ya nchini Kenya wakifundishwa na madaktari kutoka Germany Society for Tropical Pediatrics and International Child Health (GTP) jinsi ya kufanya kipimo cha kuchunguza moyo wa mtoto unavyofanya kazi (Pediatric Echocardiography). Mafunzo hayo ya siku tano yanahudhuriwa na wataalamu wa afya 22, watano kutoka Bara la Ulaya, mmoja nchini Kenya na 16 kutoka Hospitali mbalimbali hapa nchini yanatolewa na JKCI kwa kushirikiana na GTP na Chama cha madaktari wa watoto Tanzania.

Madaktari bingwa wa magonjwa ya watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  wakifundishwa na madaktari kutoka Germany Society for Tropical Pediatrics and International Child Health (GTP) jinsi ya kufanya kipimo cha kuchunguza moyo wa mtoto unavyofanya kazi (Pediatric Echocardiography). Mafunzo hayo ya siku tano yanayofanyika JKCI yanahudhuriwa na wataalamu wa afya 22, watano kutoka Bara la Ulaya, mmoja nchini Kenya na 16 kutoka Hospitali mbalimbali hapa nchini.

Daktari bingwa wa wagonjwa waliolazwa katika chumba cha uangalizi maalum (ICU) wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kiwete (JKCI)  Vivian Mlawi akifundishwa na madaktari kutoka Germany Society for Tropical Pediatrics and International Child Health (GTP)  jinsi ya kufanya kipimo cha kuchunguza moyo wa mtoto unavyofanya kazi (Pediatric Echocardiography). Mafunzo hayo ya siku tano yanatolewa na JKCI kwa kushirikiana na Shirika la Ujerumani na Chama cha madaktari wa watoto Tanzania na kuhudhuriwa na wanafunzi 22 watano kutoka Bara la Ulaya, mmoja nchini Kenya na 16 kutoka Hospitali mbalimbali hapa nchini.


Daktari  bingwa wa magonjwa ya watoto Franziska Schmidt wa Germany Society for Tropical Pediatrics and International Child Health (GTP) akifundisha wataalamu wa afya  jinsi ya kufanya kipimo cha kuchunguza moyo wa mtoto unavyofanya kazi (Pediatric Echocardiography). Mafunzo hayo ya siku tano yanahudhuriwa na wataalamu wa afya 22, watano kutoka Bara la Ulaya, mmoja nchini Kenya na 16 kutoka Hospitali mbalimbali hapa nchini yanatolewa na JKCI kwa kushirikiana na GTP na Chama cha madaktari wa watoto Tanzania.

Picha na Khamisi Mussa

Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari