Wanafunzi wa shule ya awali na msingi Libermann watoa msaada

Wahitimu wa darasa la saba 2022 shule ya awali na msingi ya Libermann wakimkabidhi moja ya zawadi mama ambaye mtoto wake amelazwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya matibabu ya moyo Pili Mwinyimkuu ikiwa ni sehemu ya kurudisha shukrani kwa jamii baada ya kumaliza salama shule ya msingi leo katika wodi ya watoto wenye magonjwa ya moyo jijini Dar es Salaam.

Wahitimu wa darasa la saba 2022 shule ya awali na msingi ya Libermann wakimkabidhi moja ya zawadi mama ambaye mtoto wake amelazwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya matibabu ya moyo Neema Ryoba ikiwa ni sehemu ya kurudisha shukrani kwa jamii baada ya kumaliza salama shule ya msingi leo katika wodi ya watoto wenye magonjwa ya moyo jijini Dar es Salaam.


Wahitimu wa darasa la saba 2022 shule ya awali na msingi ya Libermann wakimkabidhi msimamizi wa wodi ya watoto wenye magonjwa ya moyo ambaye pia ni Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Steven Lugu zawadi kwa ajili ya watoto waliolazwa katika wodi hiyo ikiwa ni shukrani kwa jamii baada ya kumaliza salama shule ya msingi.

Mkuu wa Idara ya Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Salma Wibonela akiwaelekeza wahitimu ya darasa la saba 2022 shule ya awali na msingi Libermann jinsi ya kutumia mashine ya Defibrillator inayotumika kuustua moyo pale ambapo mapigo ya moyo yapo juu sana na utendaji wake haupo vizuri walipotembelea Taasisi hiyo kwa ajili ya kutoa zawadi kwa watoto wanaotibiwa katika Taasisi hiyo ikiwa ni sehemu ya kurudisha shukrani kwa jamii baada ya kumaliza salama shule ya msingi. 

Mteknolojia mionzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Idrisa Juma akiwaonyesha wahitimu wa darasa la saba 2022 shule ya awali na msingi Libermann namna ambavyo mashine ya X-ray inafanya uchunguzi wa matatizo mbalimbali walipotembelea Taasisi hiyo kwa ajili ya kutoa zawadi kwa watoto wanaotibiwa katika Taasisi hiyo ikiwa ni sehemu ya kurudisha shukrani kwa jamii baada ya kumaliza salama shule ya msingi. 


Msimamizi wa chumba cha watoto wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum (ICU) wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Abela Venance akiwaelezea huduma zinazotolewa katika chumba hicho wahitimu ya darasa la saba 2022 shule ya awali na msingi Libermann walipotembelea Taasisi hiyo kwa ajili ya kutoa zawadi kwa watoto wanaotibiwa katika Taasisi hiyo ikiwa ni sehemu ya kurudisha shukrani kwa jamii baada ya kumaliza salama shule ya msingi. 

Mhitimu wa darasa la saba shule ya awali na msingi ya Libermann Raphael Victor akiuliza maswali wakati wahitimu hao walipotembelea Taasisi hiyo kwa ajili ya kutoa zawadi kwa watoto wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ikiwa ni sehemu ya kurudisha shukrani kwa jamii baada ya kumaliza salama shule ya msingi.

Wahitimu wa darasa la saba shule ya awali na msingi Libermann wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wazazi wao baada ya kutoa zawadi kwa watoto wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ikiwa ni sehemu ya kurudisha shukrani kwa jamii baada ya kumaliza salama shule ya msingi.

Picha na: Khamis Mussa

******************************************************************************************


Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari