Mtoto mchanga afanyiwa upasuaji wa moyo JKCI
Wataalamu wa upasuaji wa moyo kwa watoto kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
na mwenzao kutoka nchini Ujerumani Benjamin Bierbach wakimfanyia upasuaji wa kufungua
kifua mtoto mwenye umri wa mwezi mmoja na wiki tatu ambaye amezaliwa na shida
ya valvu moja ya moyo haijafunguka na chumba kimoja cha moyo hakijajitengeneza
(hakikuumbika vizuri). Upasuaji huo umefanyika katika kambi maalum ya siku tano
ya upasuaji wa moyo ambapo watoto 20 wanatarajiwa kutibiwa.
Picha na Khamisi Mussa
Comments
Post a Comment