Posts

Showing posts from May, 2023

Wapimwa viashiria vya magonjwa ya moyo kwenye Tamasha la EFM Jogging

Image
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Nnauye akimkabidhi cheti cha ushiriki wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwenye Tamasha la EFM jogging Afisa Uuguzi wa JKCI Oliver Marandu wakati wa Tamasha hilo lenye kauli mbiu Tokomeza magonjwa yasiyoambukiza lililofanyika leo katika viwanja vya Dry Morocco jijini Dar es Salaam. EFM wameandaa Tamasha hilo kwa ajili ya kuchangia damu kwa wagonjwa wanaotibiwa JKCI na Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) Maafisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwapima shinikizo la damu wadau wa jogging walioshiriki kwenye Tamasha la EFM Jogging lenye kauli mbiu Tokomeza magonjwa yasiyoambukiza lililofanyika leo katika viwanja vya Dry Morocco jijini Dar es Salaam. EFM wameandaa Tamasha hilo kwa ajili ya kuchangia damu kwa wagonjwa wanaotibiwa JKCI na Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Khairoon Mohamed akimuelezea madhara yanayoweza kusababishwa na mtindo m

Wafanyakazi wa JKCI wafanya mazoezi kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza

Image
Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), wanachama wa kikundi cha Wasafi Jogging Club pamoja na wachezaji wa Timu ya Taifa ya Cricket wakifanya mazoezi ya viungo kabla ya kuanza kwa mbio za taratibu (Jogging) za umbali wa Km. 5 ikiwa ni kampeni ya kupambana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza inayofanywa na Taasisi hiyo yenye kauli mbiu “Tembea na JKCI, Linda Afya ya Moyo Wako”.  Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), wanachama wa kikundi cha Wasafi Jogging Club pamoja na wachezaji wa Timu ya Taifa ya Cricket wakifanya mazoezi ya mbio za taratibu (Jogging) za umbali wa Km. 5 wakati wa kampeni ya kupambana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza inayofanywa na Taasisi hiyo yenye kauli mbiu “Tembea na JKCI, Linda Afya ya Moyo Wako”.    Wachezaji wa Timu ya Taifa ya Cricket wakiwaongoza Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wanachama wa kikundi cha Wasafi Jogging Club kufanya mazoezi ya mbio za taratibu (Jogging) za umbali wa Km. 5 wakati wa kampeni ya

Mkutano wa kushirikiana kitaaluma na kitafiti za afya wafanyika Poland

Image
Wageni kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili (MUHAS), Chuo Kikuu cha Rwanda na Chuo Kikuu cha Wanawake cha Ahfad Kilichopo nchini Sudani wakiwa katika mkutano wa wiki moja na viongozi wa Chuo Kikuu cha Jagiellonian cha nchini Poland kujadili namna ya kushirikiana kitaalum na kitafiti katika masuala ya afya. Wageni kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili (MUHAS), Chuo Kikuu cha Rwanda na Chuo Kikuu cha Wanawake cha Ahfad Kilichopo nchini Sudani wakitembelea maeneo mbalimbali ya Chuo Kikuu cha Jagiellonian cha nchini Poland wakati wa mkutano wa kujadili namna ya kushirikiana baina yao kitaaluma na kitafiti katika masuala ya afya *************************************************************************************************************

JKCI yasimamia mkutano wa kimataifa wa moyo

Image
Madaktari bingwa wa moyo  wawili  kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wamepata nafasi ya kushiriki katika mkutano wa Kimataifa wa EuroPCR nchini Paris kama wakaguzi wa vipindi vilivyokuwa vikiendeshwa katika Mkutano huo. Mkutano huo wa kimataifa unaofanyika kila mwaka nchini humo kuhusu upasuaji wa moyo kwa kutumia tundu dogo mwaka huu umefanyika kuanzia tarehe 15 hadi 20 Mei na kuudhuriwa na madaktari bingwa wa moyo kutoka nchi mbalimbali ambapo Tanzania iliwakilishwa na madaktari wawili wa JKCI Akizungumzia mkutano huo Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Khuzeima Khanbhai alisema katika mkutano huo moja ya mafunzo yaliyotolewa yalikuwa kuhusu interventional cardiology “Mimi pamoja na mwenzangu Dkt. Emmanuel Epafra tulipewa nafasi ya kutathmini na kuwa wakaguzi wa vipindi vilivyokuwa vikiendelea wakati wa mkutano wa EuroPCR, hii inaonyesha kuwa dunia inatuamini na kuamini huduma tunazozitoa hapa JKCI”, alisema Dkt. Khuzeima *

Wapewa mafunzo ya kuhudumia wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum na wagonjwa wanaofanyiwa upasuaji wa moyo

Image
Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo akimkabidhi cheti afisa Uuguzi kutoka Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) Agnes Msalilwa baada ya kumaliza mafunzo ya miezi sita ya namna ya kuwahudumia wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum pamoja na wagonjwa wanaofanyiwa upasuaji wa moyo yaliyomalizika hivi karibuni katika Taasisi hiyo. Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo akimkabidhi cheti afisa Uuguzi kutoka Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) Gasper Sam baada ya kumaliza mafunzo ya miezi sita ya namna ya kuwahudumia wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum pamoja na wagonjwa wanaofanyiwa upasuaji wa moyo yaliyomalizika hivi karibuni katika Taasisi hiyo. Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo akimkabidhi cheti afisa Uuguzi kutoka Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) Reinfrida Hassan baada ya kumaliza mafunzo ya miezi sita ya namna ya kuwahudu

JKCI kushirikiana na chuo kikuu cha Jagiellonian cha nchini Poland katika masuala ya afya

Image
Viongozi wa Chuo Kikuu cha Jagiellonian cha nchini Poland wakiwakaribisha wageni kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili (MUHAS) Chuo kikuu cha  Rwanda na Chuo kikuu cha Wanawake cha Ahfad kilichopo nchini Sudani kwaajili ya maandalizi ya mkutano wa wiki moja baina yao wa kujadili namna ya kushirikiana kitaaluma na kitafiti katika masuala ya Afya. *****************************************************************************************************************************  

Watu 420 wapimwa moyo Manyara

Image
Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Johnstone Kayandabila akimpima kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanyakazi (Echocardiogram – ECHO) mwananchi wa Manyara aliyefika katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Manyara (MRRH) kwa ajili ya kupima moyo wakati wa kambi maalum ya siku tano ya matibabu ya moyo iliyokuwa ikifanywa na wataalam wa afya wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa MRRH na kumalizika leo Mkoani Manyara Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Janeth Mmari akimfanyia uchunguzi mwananchi wa Manyara aliyefika katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Manyara (MRRH) kwa ajili ya kupima moyo wakati wa kambi maalum ya siku tano ya matibabu ya moyo iliyokuwa ikifanywa na wataalam wa afya wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa MRRH na kumalizika leo Mkoani Manyara Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mohamed Wamara akimpima kipimo cha kuangalia jinsi mfumo wa umeme wa moyo unavyofanya kazi (Electrocardiography – ECG) Glory Ifuny

Watoto 427 wafanyiwa uchunguzi na kupata matibabu katika kambi ya upasuaji wa moyo

Image
Wataalam wa afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao kutoka mradi wa Little Heart wa Shirika la  Muntada Aid lenye makao yake makuu mjini London nchini Uingereza wakifanya upasuaji wa kurekebisha mishipa ya damu ya moyo wa mtoto wakati wa kambi maalum ya siku tano ya upasuaji wa moyo iliyomalizika leo katika Taasisi hiyo. Wataalam wa afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao kutoka mradi wa Little Heart wa Shirika la  Muntada Aid lenye makao yake makuu mjini London nchini Uingereza wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa kambi maalum ya siku tano ya upasuaji wa moyo iliyofanyika JKCI. *************************************************************************************************************************************************************************************  Watoto 427 wenye matatizo ya matundu kwenye moyo,  matatizo ya mishipa ya damu na Valve za moyo   wamefanyiwa uchunguzi na upasuaji katika kambi maalum ya matib

Nyangasa: Kisarawe jitokezeni kupima moyo

Image
  Mkuu wa wilaya ya Kisarawe Mhe.Fatma Nyangasa akizungumza na wananchi waliofika katika h ospitali ya wilaya hiyo kwajili ya kupata huduma ya uchunguzi na matibabu ya moyo wakati wa kambi maalum ya matibabu ya siku tatu inayofanywa na wataalam wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao wa hospitali ya wilaya Kisarawe. Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya   (JKCI) Lisa Mageta akizungumza na diwani wa viti maalumu wa tarafa ya Sumn’gwi wilaya Kisarawe Valeriana Mkoka aliyefika katika hospitali ya wilaya Kisarawe   kwaajili ya kupata   huduma ya uchunguzi na matibabu ya moyo inayotolewa na wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa Kisarawe. Afisa Utafiti wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Saad Kamtoi akizugumza na mwananchi aliyefika katika Hospitali ya wilaya Kisarawe kwaajili ya kupata   huduma ya uchunguzi na matibabu ya moyo inayofanywa na wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa Kisarawe wakati wa kambi maalum ya siku tatu ya matibabu inayofa

Manyara kuwatibu wagonjwa elfu 11 wenye shinikizo la juu la damu kila mwaka

Image
Kaimu Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Manyara (MRRH) Dkt. Yesige Mutajwaa akikata utepe kuashiria maadhimisho ya siku ya shinikizo la juu la damu huku pembeni yake daktari bingwa wa moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Pedro Pallangyo akimpima shinikizo la damu Mratibu wa magonjwa yasiyoambukiza Wizara ya Afya Dkt. Anzibert Rugakingira wakati wa maadhimisho hayo yaliyofanyika kitaifa leo katika Mkoa wa Manyara  Kaimu Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Manyara (MRRH) Dkt. Yesige Mutajwaa akizungumza wakati wa maadhimisho ya siku ya shinikizo la juu la damu yaliyofanyika kitaifa leo Mkoani Manyara. Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Pima shinikizo lako la damu kwa usahihi, lidhibiti ili uishi maisha marefu”. Mratibu wa magonjwa yasiyoambukiza Wizara ya Afya Dkt. Anzibert Rugakingira akielezea namna ambavyo tatizo la shinikizo la damu linaongezeka nchini wakati wa maadhimisho ya siku ya shinikizo la juu la damu yaliyofanyika kitaifa leo Mkoani Manyara. Kauli mbiu

Tanzania yapaa kimataifa katika kutoa huduma za matibabu ya moyo

Image
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi hiyo katika hafla fupi ya kuwapongeza  madaktari bingwa wa moyo waliokwenda kutoa huduma za upimaji na matibabu ya moyo katika Hospitali ya Queen Elizabeth iliyopo nchini Malawi. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimpongeza Mkurugenzi wa Upasuaji wa Taasisi hiyo Dkt. Angela Muhozya pamoja na timu ya wataalamu wa Taasisi hiyo waliokwenda nchini Malawi katika Hospitali ya Queen Elizabeth kwaajili ya kutoa huduma za upimaji na  matibabu ya moyo. Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Peter Kisenge wakati akizungumza katika hafla fupi ya kuwapongeza madaktari bingwa wa moyo waliokwenda kutoa huduma za upimaji na matibabu katika Hospitali ya Queen Elizabeth iliyopo nchini Malawi. *********************************************************************************