Wapewa mafunzo ya kuhudumia wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum na wagonjwa wanaofanyiwa upasuaji wa moyo
Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) Dkt. Delilah Kimambo akimkabidhi cheti afisa Uuguzi kutoka
Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) Agnes Msalilwa baada ya kumaliza mafunzo ya
miezi sita ya namna ya kuwahudumia wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum pamoja
na wagonjwa wanaofanyiwa upasuaji wa moyo yaliyomalizika hivi karibuni katika
Taasisi hiyo.
Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH)
ambaye pia ni Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu wa Taasisi
ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Bashir Nyangasa akitoa neno la shukrani wakati wa
kuwaaga maafisa Uuguzi watatu kutoka BMH waliomaliza mafunzo ya miezi sita ya
namna ya kuwahudumia wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum pamoja na wagonjwa
wanaofanyiwa upasuaji wa moyo yaliyomalizika hivi karibuni katika Taasisi hiyo.
Maafisa Uuguzi wa Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) wakikata
keki wakati wa hafla fupi ya kuwaaga baada ya kumaliza mafunzo ya miezi sita ya
namna ya kuwahudumia wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum pamoja na wagonjwa
wanaofanyiwa upasuaji wa moyo yaliyokuwa yakitolewa katika Taasisi ya Moyo
Jakaya Kikwete (JKCI) na kumalizika hivi karibuni.
Comments
Post a Comment