Watoto 334 wafanyiwa uchunguzi na upasuaji wa moyo katika kambi ya matibabu inayoendelea JKCI
Watoto 334 wenye matatizo ya matundu kwenye moyo, matatizo ya mishipa ya damu na Valve za moyo wamefanyiwa uchunguzi na upasuaji katika kambi maalum ya ya siku tano ya matibabu ya moyo kwa watoto inayofanyika katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKC).
Kambi ilianza tarehe 12/05/2023 na inatarajia kumalizika tarehe 19/05/2023 inafanywa na wataalamu wa magonjwa ya moyo ya watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao kutoka mradi wa Little Heart wa Shirika la Muntada Aid lenye makao yake makuu mjini London nchini Uingereza.
Kwa muda wa siku mbili tangu kambi hiyo ianze watoto 307 wamefanyiwa uchunguzi wa moyo ambapo kati yao watoto 19 wamefanyiwa upasuaji kwa njia ya tundu dogo ambao unafanyika kwa kutumia mtambo wa Cathlab na watoto nane wamefanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo wa kufungua kifua.
Comments
Post a Comment