JKCI yasimamia mkutano wa kimataifa wa moyo
Mkutano huo wa kimataifa unaofanyika
kila mwaka nchini humo kuhusu upasuaji wa moyo kwa kutumia tundu dogo mwaka huu
umefanyika kuanzia tarehe 15 hadi 20 Mei na kuudhuriwa na madaktari bingwa wa
moyo kutoka nchi mbalimbali ambapo Tanzania iliwakilishwa na madaktari wawili
wa JKCI
Akizungumzia mkutano huo Daktari
bingwa wa magonjwa ya moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
Khuzeima Khanbhai alisema katika mkutano huo moja ya mafunzo yaliyotolewa
yalikuwa kuhusu interventional cardiology
“Mimi pamoja na mwenzangu Dkt.
Emmanuel Epafra tulipewa nafasi ya kutathmini na kuwa wakaguzi wa vipindi
vilivyokuwa vikiendelea wakati wa mkutano wa EuroPCR, hii inaonyesha kuwa dunia
inatuamini na kuamini huduma tunazozitoa hapa JKCI”, alisema Dkt. Khuzeima
*****************************************************************************************************************
Comments
Post a Comment