Manyara kuwatibu wagonjwa elfu 11 wenye shinikizo la juu la damu kila mwaka
Kaimu Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Manyara
(MRRH) Dkt. Yesige Mutajwaa akizungumza wakati wa maadhimisho ya siku ya
shinikizo la juu la damu yaliyofanyika kitaifa leo Mkoani Manyara. Kauli mbiu
ya mwaka huu ni “Pima shinikizo lako la damu kwa usahihi, lidhibiti ili uishi
maisha marefu”.
Mratibu wa magonjwa yasiyoambukiza Wizara ya Afya Dkt.
Anzibert Rugakingira akielezea namna ambavyo tatizo la shinikizo la damu linaongezeka
nchini wakati wa maadhimisho ya siku ya shinikizo la juu la damu yaliyofanyika
kitaifa leo Mkoani Manyara. Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Pima shinikizo lako la
damu kwa usahihi, lidhibiti ili uishi maisha marefu”.
Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) Pedro Pallangyo akielezea namna ambavyo JKCI imekuwa ikiwafikia
wagonjwa wa shinikizo la damu katika mikoa mbalimbali wakati wa maadhimisho ya
siku ya shinikizo la juu la damu yaliyofanyika kitaifa leo Mkoani Manyara.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Pima shinikizo lako la damu kwa usahihi, lidhibiti
ili uishi maisha marefu”.
Baadhi ya wataalam wa afya kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI), Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Manyara (MRRH) na wananchi wa
Manyara wakifuatilia hotuba zilizokuwa zikitolewa wakati wa maadhimisho ya siku
ya shinikizo la juu la damu yaliyofanyika kitaifa leo Mkoani Manyara. Kauli
mbiu ya mwaka huu ni “Pima shinikizo lako la damu kwa usahihi, lidhibiti ili
uishi maisha marefu”.
Kaimu Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Manyara
(MRRH) Dkt. Yesige Mutajwaa akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali
na wataalam wa afya kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete baada ya maadhimisho
ya siku ya shinikizo la juu la damu yaliyofanyika kitaifa leo Mkoani Manyara.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Pima shinikizo lako la damu kwa usahihi, lidhibiti
ili uishi maisha marefu”.
Na: JKCI
***********************************************************************************************************************
Wagonjwa elfu 11 wenye tatizo la shinikizo la juu la damu
hupata matibabu ya ugonjwa huo kila mwaka katika vituo vya afya vilivyopo Mkoa
wa Manyara.
Hayo yamesemwa na Kaimu Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa
Mkoa wa Manyara Dkt. Yesige Mutajwaa wakati wa maadhimisho ya siku ya shinikizo
la juu la damu yaliyofanyika kitaifa leo Mkoani Manyara.
Dkt. Yesige ambaye pia daktari bingwa wa magonjwa ya ndani
alisema idadi hiyo sio idadi kamili ya watu wenye shinikizo la juu la damu
kwani hao elfu 11 ni idadi ya wale tu wanaopata matibabu katika Mkoa huo.
“Tangu mwaka 2018 hadi 2022 mwelekeo wa shinikizo la juu la
damu kwa wananchi wa Manyara unaonyesha kuongezeka, mwaka 2018 wananchi wote
walioudhuria vituo vya kutolea huduma za afya asilimia 0.9 walikutwa na
shinikizo la juu la damu ambalo kila mwaka limekuwa likiongezeka hadi mwaka
2022 wagonjwa wa shikikizo la juu la damu walioudhuria vituo vya afya Manyara
kufikia asilimia 1.4”, alisema Dkt. Yesige
Aidha Dkt. Yesige ameishukuru Wizara ya Afya kwa kukubali na
kuuchagua mkoa wa Manyara kuwa sehemu ya maadhimisho ya siku ya shinikizo la
juu la damu kitaifa kwani kupitia maadhimisho hayo kunatoa hamasa kwa wananchi
wa Manyara kuona umuhimu wa kupima shinikizo la juu la damu mara kwa mara.
Kwa upande wake Daktari bingwa wa magonjwa ya Moyo kutoka
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Pedro Pallangyo alisema JKCI ilianzisha
kambi maalum za matibabu ya moyo lengo likiwa kusogeza huduma karibu na
wananchi, kujengeana uwezo watumishi wa afya, pamoja na kuielimisha jamii juu
ya magonjwa yasiyoambukiza.
Dkt. Pedro alisema magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo shinikizo
la juu la damu yameongezeka katika jamii hivyo ni wakati muafaka kama wadau wa
afya kupigia kelele kuipa hamasa jamii kuhusu uelewa wa magonjwa hayo ili kwa pamoja
jamii iweze kujikinga.
“Kwa kipindi cha mwaka mmoja Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
imewafikia wananchi zaidi ya elfu 8 katika mikoa ya Arusha, Geita, Mtwara,
Lindi, Zanzibar, Iringa, Dodoma, Dar es Salaam, Pwani, na Manyara ambapo watu
hao tulipowafanyia vipimo wengi tuliwakuta na shinikizo la juu la damu”,
“Wakati wa kambi hizi maalum tumekuwa tukifanya utafiti na
kubaini ya kuwa wagonjwa wanne kati ya 10 tunaowaona usumbuliwa na tatizo la
shinikizo la juu la damu”, alisema Dkt. Pedro
Kwa upande wa huduma zinazotolewa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete Dkt. Pedro aliendelea kusema kila wagonjwa saba kati ya 10 wanaofika JKCI
kwa ajili ya matibabu ukutwa na tatizo la shinikizo la juu la damu.
Naye Mratibu wa Magonjwa yasiyoambukiza Wizara ya Afya Dkt. Anzibert
Rugakingira alisema Wizara ya afya inalo jukumu la kulinda afya za watanzania hivyo
ipo mstari wa mbele kuhakikisha wananchi wanajua namba zao za shinikizo la juu
la damu, kujitambua na kupatiwa matibabu mapema.
Dkt. Rugakingira alisema nimuhimu kila mtu akawa na utaratibu
ya kupima shinikizo la juu la damu angalau mara mbili kwa mwaka ili pale mtu
anapokuwa na tatizo hilo aweze kupata matibabu kwa haraka kupunguza athari
anazoweza kupata kama hatatibiwa mapema.
Dkt. Rugakingira alisema Wizara ya Afya inao mpango wa taifa
wa kuzuia na kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo shinikizo la juu la damu,
mpango huo ulianzishwa baada ya kuwepo na ongezeko kubwa la magonjwa hayo hapa
nchini.
“Kwa muda wa kipindi cha miaka mitano utafiti umefanyika
ambapo 2017 wagonjwa wa shinikizo la juu la damu walioudhuria vituo vya afya
walikuwa laki sita na elfu themanini na nane, 2022 wagonjwa hao waliongezeka
hadi kufikia milioni moja na laki nne, wagonjwa hawa ni wale tu wanaoudhuria
kliniki naamini wapo wagonjwa wengi ambao upoteza maisha yao bila ya kufika
Hospitali kupata huduma” alisema Dkt. Rugakingira
Comments
Post a Comment