Posts

Showing posts from September, 2025

Magonjwa ya moyo: Asilimia 80 yanazuilika kwa kinga na uchunguzi wa mapema

Image
Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Peace Masaoe akimuelezea dalili za magonjwa ya moyo mwananchi aliyefika katika Hospitali ya JKCI-Dar Group iliyopo TAZARA Wilaya ya Temeke kwaajili ya kupata huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo zinazotolewa bila malipo katika maadhimisho ya siku ya moyo duniani.  Mteknolojia Maabara wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Ashura Salum akimpima sukari kwenye damu mwananchi aliyefika katika Hospitali ya JKCI-Dar Group iliyopo TAZARA Wilaya ya Temeke kwaajili ya kupata huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo zinazotolewa bila malipo katika maadhimisho ya siku ya moyo duniani.  Mfamasia kutoka kampuni ya dawa ya Hetero Labs Limited Joseph Justine akimpatia dawa mwananchi aliyefika katika Hospitali ya JKCI-Dar Group iliyopo TAZARA Wilaya ya Temeke kwaajili ya kupata huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo zinazotolewa bila malipo katika maadhimisho ya siku ya moyo duniani.  Fund...

HTAF na Vodacom kushirikiana kusaidia matibabu ya Moyo kwa watoto wenye mahitaji

Image
Mtendaji Mkuu Taasisi isiyo ya kiserikali ya Heart Team Africa Foundation (HTAF) Dkt. Naiz Majani na Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Philip Besiimire wakibadilishana hati ya mkataba wa ushirikiano wa kusaidia matibabu ya moyo kwa watoto wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) leo katika ukumbi wa JKCI iliyopo jijini Dar es Salaam.  Mtendaji Mkuu Taasisi isiyo ya kiserikali ya Heart Team Africa Foundation (HTAF) Dkt. Naiz Majani na Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Philip Besiimire wakionesha hati ya mkataba wa ushirikiano wa kusaidia watoto wenye magonjwa ya moyo wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) leo katika ukumbi wa JKCI iliyopo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa JKCI Dkt. Peter Kisenge Mtendaji Mkuu Taasisi isiyo ya kiserikali ya Heart Team Africa Foundation (HTAF) Dkt. Naiz Majani akimuelezea huduma zinazotolewa katika kliniki ya watoto wenye magonjwa ya moyo Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Philip Besiimire alipotembelea Taasisi ya ...

Mwitikio mkubwa wapelekea JKCI kuongeza siku mbili za upimaji wa Moyo bila malipo

Image
Wananchi waliofika katika Hospitali ya JKCI-Dar Group iliyopo TAZARA Wilaya ya Temeke wakisubiri kupata huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo zinazotolewa katika maadhimisho ya siku ya moyo duniani yanayofanyika katika hospitali hiyo. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na wananchi waliofika katika Hospitali ya JKCI-Dar Group iliyopo TAZARA Wilaya ya Temeke kwaajili ya kupata huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo zinazotolewa katika maadhimisho ya siku ya moyo duniani yanayofanyika leo. Mkurugenzi wa Hospitali ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group Dkt. Tulizo Shem akiwaeleza wananchi waliofika katika hospitali hiyo iliyopo TAZARA Wilaya ya Temeke huduma za matibabu wanazozitoa wakati wa maadhimisho ya   siku ya moyo duniani yanayofanyika leo ambapo hospitali hiyo inatoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo bila malipo kwa wananchi.  Afisa Lishe wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Emma...

Elimu ya Shinikizo la juu la damu yatolewa katika maonesho na madini Geita

Image
Afisa Utafiti wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Makrina Komba akimpima shinikizo la damu mwananchi aliyetembelea banda la hiyo lililopo katika Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika katika viwanja vya Maonesho vya Dkt. Samia Suluhu Hassan mjini Geita. Afisa Utafiti na Mafunzo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Zabela Mkojera akimpima urefu na uzito mwananchi aliyetembelea banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) katika Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika katika viwanja vya Maonesho vya Dkt. Samia Suluhu Hassan mjini Geita. Baadhi ya wananchi wakisubiri kupata huduma za vipimo na matibabu ya moyo walipotembelea   banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kupata huduma hizo katika Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika katika viwanja vya Maonesho vya Dkt. Samia Suluhu Hassan mjini Geita. *******************************************************************************************...

JKCI yawataka Wafamasia kutoa dawa kwa kufuata maelekezo ya Madaktari

Image
Mkurugenzi wa Idara ya magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Peter Kisenge wakati wa hafla fupi ya kuadhimisha siku ya wafamasia duniani iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam. Mkuu wa Kitengo cha Famasia wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Wellu Kaali akielezea umuhimu wa wafamasia katika jamii wakati wa hafla fupi ya kuadhimisha siku ya wafamasia duniani iliyofanyika jana katika ukumbi wa mikutano wa taasisi hiyo. Baadhi ya wafamasia wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakisikiliza wakati wa hafla fupi ya kuadhimisha siku ya wafamasia duniani iliyofanyika jana katika ukumbi wa mikutano wa taasisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Idara ya magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane akikata keki wakati  akimuwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Peter Kisenge katika hafla fupi ya kuadhimisha siku ya wafamasia d...

JKCI yawahimiza wagonjwa matumizi sahihi ya dawa

Image
Mfamasia wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Benitho Ng’ingo akitoa elimu ya matumizi  sahihi ya dawa kwa wagonjwa wanaotibiwa katika Taasisi hiyo ikiwa ni ni sehemu ya kuadhimisha siku ya Wafamasia Duniani inayofanyika  tarehe 25 Septemba. Mfamasia wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Rweyemamu Peter akiangalia dawa zinazotumiwa na mgonjwa anayetibiwa katika taasisi hiyo wakati akitoa elimu ya matumizi sahihi ya dawa ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha siku ya Wafamasia Duniani inayofanyika  tarehe 25 Septemba. Mkuu wa Idara ya Famasia wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Wellu Kaali akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafamasia wa Taasisi hiyo mara baada ya kumaliza kutoa elimu ya matumizi  sahihi ya dawa kwa wagonjwa wanaotibiwa katika taasisi hiyo  ikiwa ni ni sehemu ya kuadhimisha siku ya Wafamasia Duniani inayofanyika  tarehe 25 Septemba. Na JKCI ******************************************************************************************...

RMO Geita aipongeza JKCI kwa kutoa huduma za kibingwa za matibabu ya moyo katika maonesho ya madini

Image
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Geita (RMO) Dkt. Omary Sukari akiwa katika picha ya pamoja na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) alipotembelea banda la taasisi hiyo leo lililopo katika Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini Geita kwaajili ya kuona huduma za upimaji na matibabu ya moyo zinazotolewa na wataalamu hao. Mganga Mkuu wa Mkoa wa Geita (RMO) Dkt. Omary Sukari akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kiwkete (JKCI) lililopo katika Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojiaya Madini yanayofanyika katika viwanja vya Maonesho vya Dkt. Samia Suluhu Hassan Geita kwaajili ya kuona huduma za kibingwa za uchunguzi na matibabu ya moyo zinazotolewa. Afisa Masoko wa  Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  Agnes Mndasha akimweleza Mkemia Uchenjuaji wa  dhahabu wa Chama cha Wachimbaji wa Madini Mkoa wa Geita (GEREMA)  John Ngeda  huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo  wakati wa Maonesho ya Nane ya Kitaifa...

JKCI yazindua mfumo wa kidigitali wa miadi ya wagonjwa

Image
Afisa Tehama wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Alamin Msangi akimuelekeza mgonjwa namna ya kuchukua token katika kioski baada ya mgonjwa kufunya miadi ya kumuona daktari kupitia simu janja.  Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Tehama wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Fiona Kavishe akionesha tovuti yenye mfumo wa kidigitali wa miadi mtandao. Afisa Tehama wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Alamin Msangi akifuatilia namna ambavyo ndugu wa mgonjwa aliyelazwa JKCI anavyochukua token katika kioski kabla ya ndugu huyo kuingia kumuona mgonjwa. Na JKCI ********************************************************************************************************* Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imeanzisha mifumo miwili ya kisasa ya kuweka miadi kwa ajili ya kumuona daktari na mfumo wa namna ndugu wa mgonjwa anavyoweza kumtembelea mgonjwa aliyelazwa hospitalini. Mifumo hiyo inapatikana kupitia tovuti rasmi ya taasisi hiyo (www.jkci.or.tz) ambapo wagonjwa sasa wanaweza kuweka mi...

JKCI yatoa elimu ya Shinikizo la Juu la Damu katika maonesho ya madini G...

Image

Wananchi wapata fursa ya vipimo vya moyo katika maonesho ya madini Geita

Image
 Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Henry Mayala akimpima kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi mkazi wa Geita aliyefika katika banda la taasisi hiyo kwaajili ya kupata huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo zinazotolewa katika maonesho ya nane ya kitaifa ya teknolojia ya madini yanayofanyika kwenye Viwanja vya Maonesho vya Dkt. Samia Suluhu Hassan   vilivyopo mjini Geita. Afisa Utafiti wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Zabela Mkojera akichukua taarifa za mkazi wa Geita aliyefika katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwaajili ya kupata huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo wakati wa maonesho ya nane ya kitaifa ya teknolojia ya madini yanayofanyika katika Viwanja vya Maonesho vya Dkt. Samia Suluhu Hassan vilivyopo  mjini Geita. ***************************************************************************************************************************************************************************...

JKCI yagusa mioyo ya wanachama 125 wa TAWCA kupitia upimaji wa afya Jijini Arusha

Image
 Mwenyekiti wa Chama cha Wahasibu Wanawake Tanzania (TAWCA) CPA. Mary Mabiti akimkabidhi  jana Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Uhasibu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) CPA. Ashura Ally  tuzo ya shukrani ya utoaji wa huduma za upimaji wa magonjwa ya moyo kwa wanachama wa chama hicho waliohudhuria mkutano wa TAWCA unaofanyika jijini Arusha. Katika mkutano huo JKCI ilitoa bila malipo huduma ya upimaji wa magonjwa ya moyo kwa wanachama 125. Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Uhasibu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) CPA. Ashura Ally akigawa vipeperushi vya kutoa elimu ya magonjwa ya moyo jana kwa wanachama wa Chama cha Wahasibu Wanawake Tanzania (TAWCA) waliofika katika banda la JKCI kwaajili ya kupata huduma za upimaji wa magonjwa ya moyo inayotolewa katika mkutano wa TAWCA jijini Arusha. Afisa Lishe wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Neema Matemba akitoa elimu ya lishe bora kwa mwanachama wa Chama cha Wahasibu Wanawake Tanzania (TAWCA) aliyeshiriki mkutano wa ch...

Ujue Mfumo wa Mihadi ya kumuona Daktari na Mfumo wa kutembelea wagonjwa ...

Image

Kambi maalumu ya matibabu ya magonjwa ya mishipa ya damu kifuani kutanuk...

Image

Wanawake waaswa kulinda mioyo yao, kuepuka sukari na chumvi kupita kiasi

Image
Wahasibu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) CPA. Ashura Ally na Edna Sanga wakifuatilia mada ya wakifuatilia mada ya    kumbukumbu gani umeiacha katika eneo lako la kazi kutokana na matendo yako mazuri uliyoyafanya iliyokuwa inatolewa katika mkutano wa Chama cha Wahasibu Wanawake Tanzania (TAWCA) unaofanyika jijini Arusha. Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Idrisa Ndende akimpima kiwango cha sukari kwenye damu Mhasibu aliyefika katika banda la taasisi hiyo kwaajili ya kupata huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo wakati wa    mkutano wa Chama cha Wahasibu Wanawake Tanzania (TAWCA) unaofanyika jijini Arusha. Mkurugenzi wa Fedha na Mipango wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) CPA. Agnes Kuhenga na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo  Engerasia Kifai  wa taasisi hiyo  wakifuatilia mada ya  kumbukumbu gani umeiacha katika eneo lako la kazi kutokana na matendo yako mazuri uliyoyafanya iliyokuwa inatolewa  katika m...