Dumisheni ushirikiano kuwahudumia wagonjwa – Dkt. Kisenge
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi hiyo leo katika Ukumbi wa JKCI katika kikao cha kuangalia utekelezaji wa majukumu ya Taasisi hiyo kwa kufuata mpango mkakati wa mwaka 2022/23 – 2026/27.
Mkuu wa Kitengo cha Mafunzo na Utafiti wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Pedro Pallangyo akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2022/2023 kwa wafanyakazi wa Taasisi hiyo wakati wa kikao cha kuangalia utekelezaji wa majukumu ya Taasisi hiyo kwa kufuata mpango mkakati wa mwaka 2022/23 – 2026/27.
Baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakisikiliza taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2022/2023 wakati wa kikao cha kupitia utekelezaji wa majukumu ya Taasisi hiyo kwa kufuata mpango mkakati wa mwaka 2022/23 – 2026/27.
Afisa Tehama wa Taasisi ya moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Fiona Kavishe akielezea namna ambavyo Kitengo cha Tehama kimejipanga kuboresha huduma wakati wa kikao cha kupitia utekelezaji wa majukumu ya robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2022/2023 kwa wafanyakazi wa Taasisi hiyo kwa kufuata mpango mkakati wa mwaka 2022/23 - 2026/27.
Daktari bingwa wa usingizi na wagonjwa mahututi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Alex Loth akitoa hoja wakati wa kikao cha kupitia utekelezaji wa majukumu ya robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2022/2023 kwa wafanyakazi wa Taasisi hiyo kwa kufuata mpango mkakati wa mwaka 2022/23 - 2026/27.
Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Sulende Kubhoja akichangia mada wakati wa kikao cha kupitia utekelezaji wa majukumu ya robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2022/2023 kwa wafanyakazi wa Taasisi hiyo kwa kufuata mpango mkakati wa mwaka 2022/23 - 2026/27.
*******************************************************************************************************************************************************************************
Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wametakiwa kuendelea kudumisha ushirikiano wa kuwahudumia watanzania wenye matatizo ya moyo kwa kufanya hivyo wagonjwa watapata huduma iliyo bora zaidi.
Rai hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Peter Kisenge wakati akizungumza na wafanyakazi
hao katika kikao cha kutoa taarifa ya kazi zilizofanyika kwa kipindi cha miezi
mitatu ya Julai hadi Septemba mwaka huu.
Taarifa hiyo ya kazi inaenda sambamba na utelekezaji wa
mpango mkakati wa mwaka 2022/23 –
2025/26 ambao Taasisi hiyo imejiwekea.
Dkt. Kisenge alisema wananchi wenye matatizo ya moyo wanawategemea
wafanyakazi wa Taasisi hiyo ili wawape huduma bora ya matibabu hivyo basi
jukumu lao ni kuhakikisha wagonjwa wanaowatibu wanapata matibabu mazuri bila ya
kuwa na manung’uniko yoyote yale.
“Mnanifahamu mimi ni mchapa kazi na ninapenda kuwahudumia vizuri
wagonjwa, nitasimamia kazi ziende kama
inavyotakiwa ili Taasisi yetu iweze kufika mbali zaidi jambo la muhimu kweni ni kuwaunga mkono
viongozi wenu kwa kufanya kazi kwa ushirikiano ili malengo tuliyojiwekea yaweze
kufikiwa,”.
“Fanyeni kazi ya kuwahudumia wagonjwa kwa kufuata miongozo na
taratibu za tiba zilizopo hii ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wagonjwa wanapata
tiba sahihi na kwa wakati kwa kufanya hivyo wagonjwa hawatakaa muda mrefu Hospitali
wakisubiri kupata huduma za matibabu,” alisema Dkt.Kisenge.
Kuhusu wananchi wengi zaidi kufikiwa na huduma za kibingwa za
magonjwa ya moyo Dkt.Kisenge alisema JKCI imesogeza huduma zake kwa wananchi kwa kuwafuata mahali
walipo pia inatoa elimu kwa wataalamu wa afya walioko katika hospitali za mikoa
ya jinsi ya kufanya vipimo na kuwatambua wagonjwa wa moyo kitu ambacho
kitasaidia wagonjwa kutambulika na kuanza
matibabu mapema.
Aidha Mkurugenzi Mtendaji huyo ambaye pia ni daktari bingwa
wa magonjwa ya moyo aliiagiza Kurugenzi ya Utawala na Rasiliamali watu
kuhakikisha kila mfanyakazi anapata nakala ya mpango mkakati wa JKCI wa mwaka
2022/23-2025/2026 ili aweze kuyasoma malengo yaliyowekwa katika idara yake na kuweza kuyafanyia kazi.
Naye Mwenyekiti wa Kamati ya kusimamia utetekelezaji wa
mpango mkakati huo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Pedro
Pallangyo alisema mpango huo umefanikiwa kwa kiasi kikubwa hii imeonekana
katika taarifa ya utendaji kazi wa Taasisi hiyo zilizofanyika kwa kipindi cha
miezi mitatu ya robo mwaka wa fedha 2022/23.
“Tumeona utekelezaji wa mpango mkakati umefanikiwa katika
maeneo mbalimbali hii ikiwa ni pamoja na utoaji wa huduma za matibabu kwa
wagonjwa kwani idadi ya wagonjwa tunaowaona na kuwafanyia upasuaji imeongezeka,
Taasisi imetoa mafunzo ya jinsi ya kuwatambua wagonjwa wa moyo pamoja na
kufanya vipimo kwa wataalamu wa kada za afya kutoka hospitali mbalimbali,”.
“Kamati yetu itasimamia kila Idara ili kuhakikisha vipaumbele
walivyojiwekea vinafanikiwa pia tutahakikisha kila mfanyakazi anaufahamu zaidi mpango
mkakati huu kwa kutoa elimu ya mara kwa mara,” alisema Dkt. Pallangyo.
Kwa upande wa wafanyakazi waliohudhuria mkutano huo waliupongeza
uongozi wa JKCI kwa kusimamia mpango mkakati huo ambao umewawezesha kufanya
kazi zao za kuhudumia wananchi na
kutimiza malengo waliyojiwekea.
“Leo hii tumesomewa taarifa ya kazi tulizozifanya kwa kipindi
cha miezi mitatu na kuweza kuona kama tumefanikiwa kutimiza malengo
tuliyojiwekea au la, hiki ni kitu kizuri kwani kila mtu sasa atakuwa anafanya
kazi ili kuhakikisha malengo aliyojiwekea yanatimia jambo ambalo litaifanya
Taasisi yetu ifike mbali zaidi,” alisema Dkt. Godwin Sharau.
Comments
Post a Comment