Kikao cha kwanza cha Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete chafanyika jijini Dar es Salaam



 Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya  Kikwete (JKCI) ambaye pia ni daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu Prof. Wiliam Mahalu akiongoza kikao cha kwanza cha Bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.


 Katibu wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya  Kikwete (JKCI) ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Peter Kisenge akitoa taarifa ya utendaji wa kazi zilizofanywa na taasisi hiyo kwa kipindi cha miezi mitatu ya Julai hadi Septemba 2022 katika mwaka wa fedha wa 2022/23 wakati wa kikao cha kwanza cha Bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.


Viongozi wa Menejimenti ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi hiyo Prof. Wiliam Mahalu wakati wa kikao cha kwanza cha bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.


Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya  Kikwete (JKCI) ambaye ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Prof. Adrea Pembe akichangia mada katika kikao cha kwanza cha Bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Mjumbe wa Bodi hiyo ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Prof. Mohamed Janabi.


Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya  Kikwete (JKCI) CPA.Godfrey Kilenga kutoka ofisi ya Managing Partner TAB Consultant Audit Firm in Tanzania akichangia mada katika kikao cha kwanza cha Bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mjumbe wa Bodi hiyo Harun Matagane kutoka ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali

Comments

Popular posts from this blog

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yapata tuzo ya taasisi ambayo imetoa mchango wa kipekee kiuchumi na kijamii katika kuleta matokeo makubwa kwa kipindi cha mwaka 2023/2024

Maabara ya JKCI yapata ithibati ya kimataifa (ISO 15189:2012)