Kambi maalumu ya upasuaji wa moyo kwa watoto

                                                      TAARIFA KWA UMMA

KAMBI MAALUMU YA UPASUAJI WA MOYO KWA WATOTO


Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na mradi wa Little Heart wa Shirika la Muntada Aid lenye makao yake makuu mjini London nchini Uingereza tutafanya kambi maalumu ya upasuaji wa moyo kwa watoto tarehe 20-27/04/2024.

Kambi hii ya siku nane ambayo ni ya upasuaji mdogo wa moyo kwa njia ya tundu dogo kupitia mtambo wa Cathlab itafanyika katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo Upanga jijini Dar es Salaam.

Tunawaomba wazazi wenye watoto wanaosumbuliwa na matatizo ya moyo yakiwemo matundu, mishipa ya damu na valvu za moyo (PDA, ASD, VSD for device closure, na PS) wawalete katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi na kupatiwa matibabu.

Aidha tunawaomba madaktari kutoka Hospitali zote nchini kuwapa rufaa watoto wenye matatizo hayo ili waje JKCI kwa ajili ya kupata huduma za matibabu.

Kwa taarifa zaidi wasiliana kwa simu namba 0744-479506 Dkt. Jimmy France na 0788-308999 Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).

“Afya ya Moyo Wako ni Jukumu Letu”.

Imetolewa na:


Genofeva Matemu

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano

17/04/2024

 

 

 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari