Kambi maalumu ya upimaji na matibabu ya moyo mkoani Iringa
Afisa Lishe waTaasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Maria Samlongo na Mtaalamu wa Tiba - Viungo Jenes Blasio wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Bukoba (BRRH) wakitoa elimu ya lishe bora na umuhimu wa kufanya mazoezi kwa wananchi waliofika katika hospitali hiyo mwezi wa tatu mwaka huu kwa ajili ya kupata huduma za upimaji na matibabu ya moyo.
*********************************************************************************************************************************************************************************************************************************************************Wataalamu wa
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa (IRRH) watatoa
huduma za tiba mkoba zijulikanazo kwa jina la Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan
Outreach Services kwa kufanya upimaji na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa
wananchi wa Mkoa wa Iringa na mikoa ya
jirani.
Upimaji huu utafanyika kwa watoto na watu wazima
tarehe 15/04/2024 hadi tarehe 19/04/2024 kuanzia saa mbili kamili asubuhi
mpaka saa 10 kamili jioni katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa (IRRH).
Kutakuwa na
wataalamu wa lishe ambao watatoa elimu ya lishe bora ambayo itawapa wananchi
uelewa na kufuata mtindo bora wa maisha utakaowasaidia kuepukana na
magonjwa ya moyo ambayo ni moja ya magonjwa yasiyoambukiza na yanaweza kuepukika
kwa kufuata ushauri wa kitaalamu.
Watakaogundulika kuwa na matatizo ya
moyo watafanyiwa uchunguzi zaidi na kupatiwa matibabu hapohapo au kupewa rufaa
ya kuja kutibiwa katika Taasisi yetu.
Tunawaomba wananchi mjitokeze kwa
wingi kupima afya zenu kujua kama mna matatizo ya moyo ili kuanza matibabu mapema
kwa atakayegundulika kuwa mgonjwa.
Kwa taarifa zaidi wasiliana
kwa simu namba 0767054453 Dkt. Alfred Mwakalebela Mkurugenzi wa
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa na 0657926892 Dkt.Faith Kundy .
“Afya ya Moyo Wako ni
Jukumu Letu”.
Comments
Post a Comment