Kwa mara ya kwanza upasuaji kwa njia ya tundo dogo wa kurekebisha mishipa ya damu iliyotanuka na kupasuka kifuani na tumboni wafanyika nchini

Wataalamu wa Taasisi ya Moyo ya
Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao kutoka nchini India wakimfanyia mgonjwa upasuaji kwa njia ya tundu dogo wa kutumia
kifaa maalumu ((Stent) wa kurekebisha mshipa wa damu uliotanuka sehemu ya kifua. Wagonjwa watano watafanyiwa
upasuaji huo ambao kwa mara ya kwanza umefanyika hapa nchini kwa kutumia mtambo
wa Cathlab.
*********************************************************************************************************************************************************************************************************************Kwa mara ya kwanza wataamu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) wamefanya upasuaji kwa njia ya tundu dogo wa kurekebisha mishipa ya damu iliyotanuka na kupasuka sehemu ya kifua na tumbo kwa wagonjwa watano wenye matatizo hayo.
"Tutaendelea kutoa matibabu haya na tutaendelea kuwa na matibabu mapya mengine kwani wataalamu wetu wanajifunza kila siku. Upasuaji huu tulioufanya ukifanyika kwa njia ya kufungua kifua unachukua saa nane ila kwa njia ya tundu dogo ni saa mbili hii ni njia nzuri japo gharama ni kubwa ila Mhe. Rais wetu ametoa fedha ili wananchi wasaidiwe”, alisema Dkt.Kisenge.
Kwa upande wake daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu kutoka nchini India Gireesh Warawdekar alisema upasuaji huo unaenda sambamba na mafunzo wanayoyatoa kwa wataalamu wa JKCI ili nao waweze kuwahudumia wananchi wenye shida za mishipa ya tumbo na kifua.
“Aina hii ya upasuaji ambao tunaufanya kwa njia ya tundu dogo kwa kutumia mtambo wa Cathlab ni upasuaji mgumu lakini ni mzuri kwani hautumii muda mwingi kuufanya pia mgonjwa anayetibiwa anakaa muda mfupi hospitali na hapiti katika kipindi kigumu cha maumivu kama ilivyo kwa upasuaji wa kufungua kifua”, alisema Dkt. Warawdekar.
"Wataalmu hawa wa kutoka nchini India wapo na ujuzi mkubwa ambao wanatufundisha sisi, tunatumia mashine zetu wao wamekuja na kifaa chenye gharama kubwa kinachotengenezwa ambacho kinatumika katika upasuaji, nasi tunaelekea huko kutengeneza wataalamu watakaofanya upasuaji wa aina hii”, alisema Dkt. Angela.
Naye Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu wa JKCI Alex Joseph alishukuru ujio wa madaktari hao kutoka nchini India kwani wamefanikiwa kumfanyia upasuaji mzee wa miaka 66.
"Tulichukua saa mbili kufanyia upasuaji tulifanikiwa kwa kumuwekea kifaa maalumu (Stent) sasa hivi mgonjwa yuko vizuri ameamka na anaweza kutembea kesho anarudi kwake na upasuji wa awali wa kupasua tumbo na kifua ulikuwa na hatari kubwa ya kifo ila huu wa sasa ni salama zaidi”, alisema Dkt. Alex.
Mmoja wa wagonjwa waliofanyiwa upasuaji huo kutoka Zanzibar Ali Suleiman alisema alipata matatizo ya moyo na baada ya uchunguzi katika Hospitali ya Mnazi mmoja alibainika kuwa na matatizo ya mishipa ya damu na kupewa rufaa ya kwenda kutibiwa JKCI.
"Nimefika hapa Januari 1,2024 kulikuwa na changamoto nyingi hadi leo nimefanyiwa upasuaji, ni upasuaji mzuri kwangu nawashukuru sana madaktari wote walionifanyia upasuaji kwa usalama najisiki nina nguvu na naweza kutembea kwa miguu “.
Ninawasihi wenzangu wenye matatizo kama haya wasihangaike kwenda kutibiwa nje ya nchi waje hapa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) watatibiwa mimi nimefanyiwa upasuaji jana usiku na kama unavyoniona niko vizuri tofauti na kabla sijafanyiwa”, alisema Mzee Suleiman.
Wagonjwa wanaofanyiwa upasuaji ni wale wenye shida za mishipa ya damu kutanuka, kupasuka kwa mishipa ya damu na kuziba kwa mishipa (Aortic Aneurysm, Dissection, Peripheral artery disease).
Comments
Post a Comment