Rais wa Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud aipongeza JKCI

 

 Rais wa Jamhuri ya Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge wakati alipotembelea taasisi hiyo leo jijini Dar es Salaam kwaajili ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa.

Mkurugenzi Mtendaji  wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akimweleza Rais wa Jamhuri ya Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa na Taasisi hiyo wakati Rais huyo alipotembelea Taasisi hiyo.

Rais wa Jamhuri ya Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa  Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) mara baada ya kumaliza ziara yake ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa na Taasisi hiyo.


Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu  akimwelezea Rais wa Jamhuri ya Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud kuhusu huduma ya upasuaji mdogo wa moyo inayotolewa katika mtambo wa Cathlab wakati Rais huyo alipotembelea leo Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo jijini Dar es Salaam.

 Rais wa Jamhuri ya Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud akiangalia video fupi inayoonesha huduma zinazotolewa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati alipotembelea Taasisi hiyo leo kwaajili ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa.

 Rais wa Jamhuri ya Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud akisaini kitabu cha wageni wakati alipotembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) leo kwaajili ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa.

Rais wa Jamhuri ya Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud akizungumza na viongozi wa  Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati alipotembelea taasisi hiyo leo jijini Dar es Salaam kwaajili ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa.

**********************************************************************************************************************************************************************************************************************************

Rais wa Jamhuri ya Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud amewapongeza wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa huduma nzuri wanayoitoa ya kuokoa maisha ya watu wenye matatizo ya moyo.

Mhe. Rais Hassan Sheikh Mohamud  alizitoa pongezi hizo leo jijini Dar es Salaam alipotembelea Taasisi hiyo  (JKCI) kwaajili ya kuona  huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa.

Akiwa katika Taasisi hiyo Mhe. Rais Mahamud alitembelea maeneo mbalimbali  ya JKCI ikiwa ni pamoja na mtambo wa Cathlab ambayo ni maabara inayotumia mionzi maalumu kwaajili ya kufanya uchunguzi na matibabu  ya moyo.

Akizungumzia kuhusu ziara hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge alisema JKCI ni moja ya Taasisi inayoongoza katika nchi za Afrika Mashariki na kati katika kutoa huduma za kibingwa za matibabu ya moyo.

Dkt. Kisenge alisema Rais Mohamud alitembelea Taasisi hiyo kwaajili ya  kuona namna ambavyo nchi ya Somalia itawapeleka wagonjwa wa moyo JKCI kupata  tiba ya matibabu ya moyo.

“Nchi ya Somalia inawapeleka wagonjwa wengi  wa moyo kwenda kutibiwa katika nchi za India, Ulaya na Marekani  wakati huduma hii inapatikana nchini Tanzania, na ukiangalia nchi hizi ziko karibu hivyo basi itakuwa ni rahisi kwao kuwaleta wagonjwa kuja kutibiwa hapa kwetu”.

“Kuja kwa wagonjwa hawa kutaisaidia nchi yetu kukua kiuchumi kwani pesa zitakazopatikana zitawafikia watu wengi ikiwemo wamiliki wa hoteli ambako wagonjwa watalala pamoja na wafanyabiashara watakaowauzia vyakula na mahitaji mengine”, alisema Dkt. Kisenge.

 Dkt. Kisenge alimshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuzidi kuimarisha mahusiano na nchi za nje ndiyo maana watu wengi wanakuja kuwekeza hapa nchi hata Taasisi hiyo imekuwa ikiwapokea  wageni mbalimbali kutoka nchi za nje.

Akiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mhe. Rais Hassan Sheikh Mohamud pamoja na ujumbe wake aliambata na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu.


Comments

Popular posts from this blog

Wataalamu wa JKCI kufanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

JKCI na AICC Hospitali kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo katika kikao kazi cha wenyeviti na watendaji wakuu wa Taasisi za Umma

JKCI yamshukuru Rais Dkt.Samia kwa kuwapa magari