Viongozi watembelea banda la JKCI maonesho ya Osha
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Ajira Vijana na
Wenye Ulemavu Mhe. Deogratius Ndejembi akizungumza na Daktari bingwa wa moyo wa
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dickson Minja alipotembelea banda la
Taasisi hiyo wakati wa kambi maalumu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach
Services katika maonesho ya kimataifa ya usalama na afya mahali pa kazi
yanayofanyika viwanja vya General tyre jijini Arusha.
Mkurugenzi Mkuu Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Dkt.
John Mduma akipimwa shinikizo la damu na Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) Odilia Njau alipotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa kambi
maalumu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach Services katika maonesho ya
kimataifa ya usalama na afya mahali pa kazi yanayofanyika viwanja vya General
tyre jijini Arusha.
Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Benson
Bisare akimwelezea mwananchi uhusiano kati ya urefu na uzito mara baada ya
kupima uzito wakati wa kambi maalumu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach
Services katika maonesho ya kimataifa ya usalama na afya mahali pa kazi
yanayofanyika viwanja vya General tyre jijini Arusha.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Highridge iliyopo jijini Arusha
wakimsikiliza daktari bingwa wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
Dickson Minja alipokuwa akiwafundisha jinsi moyo unavyofanya kazi wakati wa
kambi maalumu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach Services katika
maonesho ya kimataifa ya usalama na afya mahali pa kazi yanayofanyika viwanja
vya General tyre jijini Arusha.
Na: JKCI
*********************************************************************************************************
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imepongezwa kwa kusogeza
huduma karibu na wananchi na kuwafanyia uchunguzi na matibabu ya moyo wananchi
wa mkoa wa Arusha.
Pongezi hizo zimetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri
Mkuu Kazi Ajira Vijana na Wenye Ulemavu Mhe. Deogratius Ndejembi alipotembelea
banda la Taasisi hiyo wakati wa kambi maalumu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan
Outreach Services katika maonesho ya kimataifa ya usalama na afya mahali pa
kazi yanayofanyika viwanja vya General tyre jijini Arusha.
Mhe. Ndejembi alisema JKCI imekuwa ikifanya vizuri katika
kutoa huduma za matibabu ya moyo nchini na kuwa kimbilio kwa wananchi wengi
wenye magonjwa ya moyo.
“Nawapongeza kwa kazi nzuri mnayoifanya, JKCI naijua vizuri
kutokana na huduma zake za kipekee inazozitoa za matibabu ya moyo hapa nchini”,
alisema Mhe. Ndejembi.
Akizungumza mara baada ya kutembelea banda la JKCI Mkurugenzi
Mkuu Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Dkt. John Mduma alishukuru kwa
kupatiwa huduma za uchunguzi wa afya na ushauri kutoka kwa wataalamu wa afya.
“Nawashukuru wataalamu wa afya wa JKCI kwa kunipa nafasi ya kupima
afya yangu lakini hamkuishia hapo bali mmeweza pia kunipa elimu kuhusu mfumo
bora wa maisha”, alisema Dkt. Mduma
Kwa upande wake Mkurugenzi wa shule ya msingi Highridge Adam
Washokera alisema alipofika katika banda hilo na kupatiwa huduma aliona kuna
fursa ya kuwaleta wanafunzi wa shule yake kujifunza kuhusu moyo kwani ni vitu
ambavyo wanafunzi wanajifunza darasani.
“Baada yakufika katika banda hili na kupatiwa huduma niliona
fursa ya kuwaleta wanafunzi wa darasa la nne na la saba kujifunza kuhusu moyo
kutoka kwa daktari bingwa wa moyo kwani daktari anaujua moyo vizuri hivyo
watoto wamepata elimu kwa vitendo”, alisema Adam
Adam alisema baadhi ya wanafunzi wamekuwa na ndoto ya kuwa
madaktari hivyo wakisogezwa karibu na watu wa ndoto zao wanapata motisha zaidi
kusoma na kufikia ndoto zao.
Naye mwananfunzi wa darasa la saba shule ya msingi Higridge
Joshua Proches alisema amefurahi kufika katika banda la JKCI kupata elimu na
kujua nini kinachosababisha mtu kupata magonjwa ya moyo.
“Nimekuwa nikisikia watu wanaumwa moyo lakini sikuwa najua
moyo unaumwa vipi na nini kinasababisha moyo kuumwa lakini baada ya kupata
elimu kutoka kwa daktari nimejua”, alisema Joshua
Comments
Post a Comment