Kliniki ya JKCI iliyopo SABASABA yaanza kutoa huduma kwa wananchi

Baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.

Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Nyanjura Nyaruga akimpima kiwango cha sukari kwenye damu mwananchi aliyetembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.

Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Happy Malunde akiwaelezea huduma zinazotolewa katika chumba cha upasuaji wa wananchi waliotembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.

Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Nyanjura Nyaruga akimpima shinikizo la damu mwananchi aliyetembelea banda la JKCI wakati wa maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.


Mfamasia wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dorothea Simkwai akimpatia dawa mwananchi aliyetembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA) yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.

Na JKCI

*********************************************************************************************

Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kupitia kliniki yake iliyopo katika maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (SABASABA) yaanza kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa wananchi wanaotembelea katika maonesho hayo.

Kupitia kliniki hiyo wananchi wanapimwa shinikizo la damu, sukari kwenye damu, mafuta kwenye damu, kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiography), na kipimo cha kuangali mfumo wa umeme wa moyo (Electrocardiogram - ECG).

Vipimo vingine vinavyofanyika katika banda hilo ni vipimo vya maabara pamoja na kutoa chanjo ya homa ya ini. Aidha wananchi wanaotembelea banda la JKCI wanapata fursa ya kupata ushauri kuhusu lishe bora kutoka kwa wataalamu waliobobea katika lishe.

Ili kuboresha afya za wananchi JKCI imepanga kutumia maonesho hayo kama sehemu ya kuongeza jitihada dhidi ya kinga ya magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo ya moyo kutokana na magonjwa hayo kuongezeka na kupunguza nguvu kazi ya taifa.

Sambamba na kauli mbiu ya maonesho hayo JKCI imejipanga kuwa fahari ya Tanzania kupitia maonesho ya 50 ya SABASABA kwa kutoa huduma bora kwa kila mwananchi atakayetembelea banda hilo.


Comments