Wanafunzi 2,328 wapimwa moyo Kibaha
Daktari bingwa wa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya kikwete (JKCI) Theophil Ludovic akiwafundisha wanafunzi wa Shule ya Msingi Mailimoja kuhusu magonjwa ya moyo kwa watoto wakati wa kambi maalumu ya siku mbili ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tiba mkoba iliyokuwa ikifanywa na Taasisi hiyo katika maadhimisho ya miaka 10 ya JKCI tangu kuanzishwa kwake. Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya kikwete (JKCI) Stella Mongela akimpima kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiography) mwanafunzi wa Shule ya Msingi Mailimoja wakati wa kambi maalumu ya siku mbili ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tiba mkoba iliyokuwa ikifanywa na Taasisi hiyo katika maadhimisho ya miaka 10 ya JKCI tangu kuanzishwa kwake. Wanafunzi wa Shule ya Msingi Mailimoja wakiwa katika foleni ya kufanyiwa uchunguzi wa magonjwa ya moyo wakati wa kambi maalumu ya siku mbili ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tiba mkoba iliyokuwa ikifanywa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ka...