Wagonjwa 12,180 kutoka nje ya nchi watibiwa Tanzania

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalage akizungumza wakati wa mdahalo wa wazi wa kitaalamu kuhusu utalii tiba nchini ulioandaliwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) katika kuadhimisha miaka kumi tangu kuanzishwa kwake leo katika Ukumbi wa Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Mkurugenzi Mtendaji Hospitali ya Benjamini Mkapa Prof. Abel Makubi akimsikiliza mtaalamu kutoka Kampuni ya Sakaar Healthtech Limited Alfred Moshi akimuelezea kuhusu kifaa maalumu kijulikanacho kwa jina la Dozee kinachotumika kufuatilia maendeleo ya mgonjwa anayetibiwa akiwa nyumbani wakati wa mdahalo wa wazi wa kitaalamu kuhusu utalii tiba nchini ulioandaliwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) katika kuadhimisha miaka kumi tangu kuanzishwa kwake leo katika Ukumbi wa Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).


Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) akizungumza wakati wa mdahalo wa wazi wa kitaalamu kuhusu utalii tiba nchini ulioandaliwa na Taasisi hiyo katika kuadhimisha miaka kumi tangu kuanzishwa kwake leo katika Ukumbi wa Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Dkt. Delilah Kimambo akichangia mada wakati wa mdahalo wa wazi wa kitaalamu kuhusu utalii tiba nchini ulioandaliwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) katika kuadhimisha miaka kumi tangu kuanzishwa kwake leo katika Ukumbi wa Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Wadau wa Sekta ya Afya wakisikiliza wakati wa mdahalo wa wazi wa kitaalamu kuhusu utalii tiba nchini ulioandaliwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) katika kuadhimisha miaka kumi tangu kuanzishwa kwake leo katika Ukumbi wa Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalage Akiwa katika picha ya pamoja na viongozi na wanafunzi wa Shule za Sekondari wakati wa mdahalo wa wazi wa kitaalamu kuhusu utalii tiba nchini ulioandaliwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) katika kuadhimisha miaka kumi tangu kuanzishwa kwake leo katika Ukumbi wa Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Na: JKCI

*****************************************************************************************************

Wagonjwa 12,180 kutoka nje ya nchi wametibiwa nchini kati ya mwaka 2021 hadi 2025 na kuongeza fursa za utalii tiba nchini.

Akizungumza wakati wa Mdahalo wa wazi wa kitaalamu kuhusu utalii tiba nchini Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe alisema ongezeko la wagonjwa hao kutoka 5,700 hadi kufikia 12,180 kwa kipindi cha miaka mitano limetokana na mipango mikakati ya uwekezaji mkubwa uliofanywa na serikali.

Dkt. Shekalaghe alisema lengo la uwekezaji wa utalii tiba nchini ni kutaka kufikia uchumi   wa kati na kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha tiba utalii Afrika.

"Wizara ya Afya imeandaa muongozo wa tiba utalii nchini unaoainisha mambo muhimu ya kuzingatia na itaendelea kutoa ufadhili wa masomo kwa wataalamu kuputia Samia Scholarship hivyo tunategemea wataalamu kutoka katika Taasisi zinazotoa huduma bingwa bobezi kama ya moyo watakuwepo", alisema Dkt. Shekalaghe.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Diplomasia kutoka Wizara ya Mambo ya Nje Mhe. Balozi John Ulanga alisema kumekuwa na ongezeko la utalii tiba kwa asilimia 19 ambao  imeongeza pato la taifa kufikia Shilingi Bilioni 166.5 .

Mhe. Balozi Ulanga alisema Tanzania inapokea wagonjwa kutoka katika nchi  16 za Afrika zikiwemo Comoro, Burundi, Zambia, DRC Congo, Kenya, Uganda na nyinginezo.

"Kuanzia 2021 hadi 2025 kumekuwa na ukuaji mkubwa wa huduma zinazotolewa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI), Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), hHospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) na Hospitali ya Saratani ya Ocean Road”, alisema Mhe. Balozi Ulanga

Mhe. Balozi Ulanga alisema ifikapo mwaka 2030 Tanzania inategemea kuwa na watalii wa matibabu 30,000, mwaka 2040  watalii wa matibabu 68,000 na  mwaka 2050 watalii wa matibabu 120,000  watakaotaka kufika Tanzania kupata huduma za kibingwa na bobezi.

“Kwa mantiki hiyo mwaka 2030 tunauwezo wa kufika dola za Kimarekani milioni 200, mwaka 2040 tunaweza kupata dola za Kimarekani milioni 420, na mwaka 2050 tunaweza kupata dola za Kimarekani milioni 850”, alisema Mhe. Balozi Ulanga.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge alisema asilimia 99 ya wagonjwa wa moyo nchini sasa wanatibiwa ndani ya nchi ambapo kiasi cha shilingi bilioni 95 zimeokolewa kama wagonjwa hao wangeenda nje ya nchi.

"Hadi sasa tumefikia mikoa 23 katika programu yetu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach Services ambapo wananchi wengi wamepata huduma za uchunguzi wa magonjwa ya moyo. Pia tumefungua matawi ya JKCI Oysterbay, Kawe, Dar Group, Hospitali ya Chato na kuingia makubaliano na Hospitali ya Seliani iliyopo Arusha kwaajili ya kuwatibu wagonjwa wa moyo”, alisema Dkt. Kisenge.












 

Comments

Popular posts from this blog

Wateja wa CRDB kutibiwa JKCI kwa punguzo la asilimia 50%

Wanawake wa JKCI SACCOS wanaongoza kwa kumiliki hisa

JKCI, MOI NA MNH waitwa Comoro kutoa huduma za matibabu ya kibingwa