JKCI yasherehekea miaka 10 kwa mdahalo wa Utalii wa Matibabu


Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Amanda Anyoti akiwaeleza wananchi wa Zambia jinsi moyo unavyofanya kazi wakati wa maonesho ya 97 ya Kilimo na Biashara ya Zambia yaliyomalizika hivi karibuni jijini Lusaka. JKCI ilishiriki maonesho hayo kwa kwenda kutangaza huduma za matibabu ya ubingwa bobezi ya moyo inazozitoa.

Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Alex Joseph akimpima Shinikizo la damu mkazi wa Zambia aliyefika katika banda la taasisi hiyo  kwaajili ya kupata huduma ya uchunguzi wa awali wa magonjwa ya moyo  wakati wa maonesho ya 97 ya Kilimo na Biashara ya Zambia yaliyomalizika hivi karibuni jijini Lusaka. JKCI ilishiriki katika maonesho hayo kwa kwenda kutangaza huduma za matibabu ya ubingwa bobezi ya moyo inazozitoa.

********************************************************************************************************************************************************************************

Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imeandaa mdahalo wa Utalii wa Matibabu wenye lengo la kutoa elimu kwa umma kuhusu mchango wa taasisi hiyo katika kuboresha huduma za afya ya moyo na mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kipindi cha miaka kumi tangu kuanzishwa kwake.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa Kamati ya maadhimisho ya miaka 10 ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt.  Naiz Majani alisema mdahalo huo utafanyika katika ukumbi wa maktaba mpya uliopo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) tarehe 15 mwezi huu kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa sita mchana.

Dkt. Naiz ambaye pia ni Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa JKCI alisema Serikali imeboresha miundombinu ya afya hii ikiwa ni pamoja na upatikianaji wa  huduma bora za afya za ubingwa bobezi na hivyo kuwafanya watu wengi kutoka nje ya nchi kuja kutibiwa nchini na kukuza uchumi wa taifa.

“Katika mdahalo huu tutajadili  utalii wa matibabu na manufaa yake kwa mtanzania mmoja mmoja, utalii wa matibabu Afrika: Tulikotoka, tulipo na tunakoelekea, nafasi ya Mashirika ya Umma katika kukuza utalii wa matibabu Tanzania na tulipofikia Tanzania katika utalii wa matibabu”.

“Utalii wa matibabu ni fursa ya kipekee kwa watanzania wote kukuwa kiuchumi kuanzia wamiliki wa magari ya usafirishaji, wajasiriamali wa chakula hadi watoa huduma za malazi watakapofikia wageni kutoka nje ya nchi ambao watakuja kutibiwa hapa nchini”, alisema Dkt. Naiz.

Dkt. Naiz aliwaomba wananchi kujitokeza kwa wingi katika mtahalo huo ili wajifunze namna ambavyo tiba utalii inavyoweza kuboresha maisha yao na kuinua uchumi wa taifa.

Comments

Popular posts from this blog

Wateja wa CRDB kutibiwa JKCI kwa punguzo la asilimia 50%

Wanawake wa JKCI SACCOS wanaongoza kwa kumiliki hisa

JKCI, MOI NA MNH waitwa Comoro kutoa huduma za matibabu ya kibingwa